Thursday, March 14, 2019

Ukatili







Ukatili sio tu msamiati wa lugha ya Kiswahili, bali hutumiwa kuashiria maovu ambayo yanazidi kuongezeka katika jamii kila siku. 


Ukatili ni hali ya kutokuwa na huruma. Ukatili wa kijinsia ni kitendo anachofanyiwa mtu yeyote mwanamke au mwanamme kwa lengo la kumdhuru au kumuumiza kisaikolojia, kimwili, kiafya, kingono na kiuchumi.

Tafiti nyingi zinaonyesha kwamba wanawake ndio wahanga wakubwa wa ukatili wa jinsia.

Visa vya ukatili vimeongezeka humu nchini katika siku za hivi karibuni, kutokana na kuongezeka kwa ripoti za mume kumuua mkewe, mke kumuua mumewe au watoto kuuawa na baba au mama na hata watoto kunajisiwa.

 
Ukatili husababishwa na mambo mengi, ikiwemo kutoelewana, hasira, chuki, matatizo ya kifedha, kupoteza kazi, kutaka kuonekana kudhibiti familia, na matumizi ya pombe na mihadarati.


Kwa mujibu wa Bibilia kwenye kitabu cha Methali 15 moja, jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu.

No comments:

Post a Comment

Emotions of the Game!

Football just like other sports brings a tidal of emotions and feelings when it happens.Its never a surprising scene to see a kid breakdown ...