Governor wa Kisumu Profesa Peter Anyang' Nyong'o amefungua rasmi
kongamano la kimataifa kuhusu makazi ya kutosha na gharama ya chini.
kongomano
hilo ambayo imepangwa na shirika la Grassroot Trust ikiungana na kaunti
ya Kisumu imeng'oa nanga hivi leo hadi siku ya Alhamisi ambapo
inatarajiwa kufungwa rasmi na Mheshimiwa Raila Odinga.
Akizungumza
kwenye kongamano hilo Nyong'o amesema kuwa wanaendeleza mipango za
kuimarisha makazi jijini kisumu wakiungana na mashirika zisizo za
serikali ili kuhakikisha kwamba wakazi wa kisumu wanaishi kwa nyumba
zenye gharama za chini,zenye usalama na maji,na vituo vya afya.
Wageni
wengi kutoka ugaibunu pamoja na wakazi wa kisumu wamehudhuria kongomano
hilo inayofanyika kwenye hoteli ya kifahari ya Grand Royal Swiss
iliyoko eneo ya Riat jijini Kisumu .
Lawrence Apiyo ambaye ni mshirikishi wa shirika la Grassroot trust akizungumza amesema kwamba wanafanya juhudi kama shirika kuhakikisha wakazi wa kisumu wanaishi kwa nyumba nzuri.
No comments:
Post a Comment