Nyumba na makazi bora ni mojawapo kati ya agenda nne kuu za rais Uhuru Kenyatta...
Lakini
wakenye wengi bado wanaishi kwenye nyumba duni zenye mazigira
chafu,kukosa maji,kutokuwa na hospitali,ukosefu wa usalama na mashida
zinginezo.
Nilipotembea mtaani Bandani iliyoko
jijini Kisumu tulisuhudia baadhi ya nyumba ambazo hali zao si nzuri kwa
afya ya binadamu yeyote yule.Baadhi ya nyumba hizo hazina hata vyoo kwa
hivyo wanaoishi huko wanahatarisha maisha yao kwa kulipa pesa kiasi.
Nilipozungumza
na kikundi cha project comitee management{pmc}ambao wanafanya juhudi na
mradi ya ujenzi wa nyumba za matofali ili angalua kuinua hali ya maisha
ya wanaoishi Bandani wamesema chama yao inalenga kuhakikisha kwamba wakazi wa Bandani wanaishi kwa nyumba bora kwa siku za usoni.
Mwenyekiti wa
PMC Bwana Abubakar Hasan Makengeza amesema kuwa serikali ya kaunti ya
kisumu imewapa machine ya kutengeneza matofali kwa hivyo wao hutengeneza
takriban matofali alfu moja kwa siku.
Ameongeza kwamba wako na kamati ya watu sita ambao wanongeza kikundi cha kuhakikisha kwamba wakazi wa bandani wataishi kwa nyumba nzuri.
No comments:
Post a Comment