Mechi tatu za ligi kuu ya soka nchini-KPL,zimechezwa hivi leo.
Kariobangi Sharks wametoka sare ya bao moja kwa moja dhidi ya zoo kericho kwenye uga wa Nairobi City.
Sofapaka nao pia wametoka sare ya bao moja kwa moja dhidi ya Vihiga United kwenye uga wa Nyao jijini nairobi.
Nzoia
sugar wametesa nyasi bure dhidi ya posta rangers na kutoka na sare ya
kutokuwa na bao kwenye uga wa Masinde Muliro BUngoma.
Huko AFC Leopards almaarufu Ingwe wakishinda Chemelil Sugar kwa mabao mawili kwa sufuri kwenye uga wa Nyanyo jijini Nairobi.